Tanzania vs Nigeria mchezo wa kwanza AFCON 2025Bendera

Tanzania vs Nigeria mchezo wa kwanza AFCON 2025 kwa timu hizi kutupa karata uwanjani. Ni Desemba 23 wawili hawa kutoka kundi C watakuwa uwanjani kusaka ushindi. Tayari Taifa Stars imewasili inayofundishwa na Miguel Gamondi ipo Morocco kwa maandalizi ya mwisho kwenye mashindano haya makubwa.  

SOMA HII: AFCON 2025: Joto lapanda Morocco, Jeshi la Tanzania laweka kambi Misri

Zamu yako kushinda sasa hivi, cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni

Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

image

Ni Tanzania vs Nigeria mchezo wa kwanza AFCON 2025, ratiba ipo hivi

Tanzania vs Nigeria mchezo wa kwanza AFCON 2025
Mbwana Samatta nahodha wa Taifa Stars. Source: Taifa Stars.

Nchini Morocco, Tanzania vs Nigeria mchezo wa kwanza AFCON 2025 kwa timu hizi kutoka kundi C. Baada ya mchezo huo zipo mechi nyingine kali zitachezwa. Ratiba inaonyesha kuwa mchezo wa kwanza kwa Taifa Stars utachezwa saa 2:30 usiku. Desemba 27 itakuwa ni Tanzania vs Uganda, saa 2:30 usiku na Desemba 30 Tanzania vs Tunisia saa 1:00 usiku.

Haya hapa makundi ya AFCON 2025

Kundi A

Morocco, Mali, Zambia, Comoros

Kundi B

Misri, Afrika Kusini, Angola, Zimbabwe

Kundi C

Nigeria, Tunisia, Uganda, Tanzania

Kundi D

Senegal, DR Congo, Benin, Botswana

Kundi E

Algeria, Burkina Faso, Guinea ya Ikweta, Sudan

Kundi F

Ivory Coast, Cameroon, Gabon, Msumbiji

SOMA HII: Hawa hapa wachezaji 5 wa kuchungwa AFCON 2025 Morocco

image

Kambi Taifa stars ilianzia Misri

Fei Stars
Fei Toto nyota wa Taifa Stars. Source: Taifa Stars.

Kikosi cha Taifa Stars kabla ya kuelekea Morocco kwanza kiliweka kambi ya muda nchini Misri. Mbinu za Kocha Mkuu Miguel Gamondi zilianza kufundishwa hapo. Lengo la kambi hiyo ilikuwa ni kupata mazingira bora ya mazoezi.

Bendera mikononi mwa Stars

Desemba 18, 2025 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paramagamba Kabudi alikabidhi bendera ya Taifa kwa timu ya Taifa kwa kwa ajili ya kuelekea Morocco kwenye Fainali za AFCON 2025. Desemba 19,2025 kikosi cha Stars kiliwasili nchini Morocco kwa maandalizi ya mwisho.

Mbwana Samatta kambini

Nahodha Mbwana Samatta aliwasili kambini nchini Misri Desemba 17. Aliungana moja kwa moja na wachezaji wengine kwa maandalizi zaidi. Mbali na Samatta winga Simon Msuva naye ni miongoni mwa wachezaji ambao wapo kwenye kikosi.

Mazoezi yaanza Morocco

Mara baada ya kuwasili nchini Morocco timu hiyo ilipata muda wa kufanya mazoezi. Ni kwenye Uwanja wa Academic Mohammed VI, Rabat, Morocco waliutumia kwa mazoezi. CAF Total Energies AFCON 2025 inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Mwalimu ajumuishwa fasta

Kocha Miguel Gamondi amemuita mshambuliaji Selemani Mwalimu kwenye kikosi cha wachezaji 28. Awali mshambuliaji huyo hakuwa kwenye orodha ya watakaocheza AFCON 2025 Morocco. Mwalimu alichagulikuwa kuchukua nafasi ya Abdul Suleiman wa Azam FC ambaye aliumia hiyo ilikuwa Desemba 13,2025.

SOMA HII: Yanga SC hawana utani wamerejea kazini 2025/26/ Orodha ya wachezaji waliopo AFCON

image

Kikosi cha Taifa Stars

Yakoub Suleiman- Simba SC

Hussen Masalanga-Singida Black Stars

Zuber Foba-Azam FC

Bakari Nondo- Yanga SC

Shomari Kapombe-Simba SC

Lusajo Mwaikenda-Azam FC

Mohamed Hussen- Yanga SC

Nickson Kibabage- Singida Black Stars

Alphonce Mabula-Shamakhi , Azerbaijan

Wilson Nangu- Simba SC

Novatus Dismas-Goztepe FC, Uturuki.

Kelvin Nashon-Pamba Jiji

Pascal Msindo-Azam FC

Ibrahim Abdallah- Yanga SC

Haji Mnoga-Salford City, Uingereza

Dickson Job- Yanga SC

Habib Idd- Singida Black Stars

Tarryn Allarakha- Rochdale AFC, Uingereza

Charles M’mombwa- Floriana FC, Malta

Yusuph Kagoma- Simba SC

Feisal Salum- Azam FC

Morice Abraham- Simba SC

Seleman Mwalimu- Simba SC

Idd Suleiman- Azam FC

Kibu Dennis- Simba SC

Mbwana Samatta- Le Havre AC, Ufaransa.

Kelvin John-Aalborg BK, Denmark

Simon Msuva-Al-Talaba, Iraq

Wachezaji stars
Wachezaji wa Taifa Stars nchini Morocco. Source: Taifa Stars.

Hitimisho

Tanzania vs Nigeria mchezo wa kwanza AFCON 2025 ni mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa. Wababe hawa kutoka kundi C kila mmoja anahitaji kufungua pazia kwa ushindi. Je nani ataanza kwa kicheko? Endelea kufuatilia ukurasa huu matokeo utayapata mara baada ya mchezo kutamatika.

Share this: