- Yanga SC vs Simba SC kituo kinachofuata Machi Mosi, New Amaan Complex
- Dodoma Jiji FC vs Simba SC ni leo NBC Premier League Februari 25,2026 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma
- Steve Barker Kocha Mkuu wa Simba SC akiri ugumu wa mchezo
Dodoma Jiji FC vs Simba SC ni ratiba ya leo NBC Premier League 2025/26. Mnyama anakuwa ugenini Uwanja wa Jamhuri, Dodoma saa 1:15 usiku. Baada ya mchezo wa leo kituo kinachofuata itakuwa Yanga SC vs Simba SC, Machi Mosi 2026, Uwanja wa New Amaan Complex.
SOMA HII: Tanzania Prisons 0-2 Simba SC NBC Premier League/ Highlights, statistics, standings
Cheza na ushinde sasa na ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni muda huu
Zamu yako kushinda na SportPesa, unaweza kushinda mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kupitia Kampuni bora ya michezo ya kubashiri ya SportPesa bonyeza picha hii chini.

Dodoma Jiji FC vs Simba SC utabiri unasemaje?

Kuelekea mchezo wa Dodoma Jiji FC vs Simba SC utabiri unamuangikia mnyama kwa ushindi. Hii inatokana na rekodi ya mechi za ugenini kupata ushindi asilimia 100. Licha ya Simba SC kupewa asilimia kubwa kushinda bado Dodoma Jiji FC sio timu ya kubeza.
SOMA HII: Timu tano zilikuwa na maajabu ya sabasaba | Yanga SC na Simba SC zatuma ujumbe maalumu

Msimamo Dodoma Jiji FC vs Simba SC
| MP | W | D | L | PTS | |
| 4. Simba SC | 9 | 7 | 1 | 1 | 22 |
| 6.Dodoma Jiji FC | 15 | 5 | 5 | 5 | 20 |
Matokeo yaliyopita kwa Simba SC
Februari 22,2026 Tanzania Prisons 0-2 Simba SC
Matokeo yaliyopita kwa Dodoma Jiji FC

Februari 12,2026 Dodoma Jiji FC 3-0 TRA United
Maoni ya kocha wa Dodoma Jiji
Amani Josiah, kocha wa Dodoma Jiji FC amebainisha wamefanya maandalizi vizuri. Kocha huyo ameongeza kuwa wanawaheshimu wapinzani wao watawakabili kwa nidhamu.
“Tunawaheshimu wapinzani wetu Simba SC tutawakabili kwa nidhamu kubwa. Tumefanya maandalizi mazuri kimwili, kiakili, kimbinu na hasa kisaikolojia,” alisema Josiah.
Rekodi zinaonyesha Dodoma Jiji FC wamecheza mechi 7 wakiwa nyumbani, ushindi mechi 4, sare 2 ikipoteza mchezo nmoja.
SOMA HII: Yanga SC vs JKT Tanzania NBC Premier League/ Ahmed Ally, Pedro watambiana/ Ratiba, msimamo

Maoni ya Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker
Kocha wa Mkuu wa Simba SC, Steve Barker amebainisha kuwa watajithidi kucheza kwa umakini mbele ya wapinzani. Amebainisha kuwa anatambua watakutana na ugumu.
“Tumejiandaa na ugumu tutakaokutana nao kwenye mchezo wetu dhidi ya Dodoma Jiji FC. Tutajitahidi kucheza kwa malengo ili kupata matokeo mazuri,” alisema Barker.
Simba SC ikiwa ugenini NBC Premier League 2025/26 imecheza mechi 3, ilipata ushindi mechi zote 3 ikivuna pointi 9.

H2H
14/03/2025, Simba SC 6-0 Dodoma Jiji FC
29/09/2024, Dodoma Jiji FC 0-1 Simba SC
17/05/2024, Dodoma Jiji FC 0-1 Simba SC
01/10/2021, Dodoma Jiji FC 0-1 Simba SC

Hitimisho
Dodoma Jiji FC vs Simba SC ni mchezo muhimu kwa timu zote mbili uwanjani. Mara baada ya ratiba ya leo kukamilika kituo kinachofuata kwa mnyama ni Kariakoo Dabi.Yanga SC vs Simba SC inatarajiwa kuchezwa Machi Mosi, 2026, Zanzibar.

