Yanga SC yaibana mbavu JS Kabylie CAF Champions LeagueDiarra tena (-)
  • Highlights Novemba 28, 2025 JS Kabylie 0-0 Yanga SC mechi ya pili kati ya 6 kundi B.
  • Yanga SC yaibana mbavu JS Kabylie CAF Champions League 2025/26.
  • Azam FC 0-1 Wydad Casablanca Caf Cofideration Cup, Aziz Ki akimbizwa hospital.

Yanga SC yaibana mbavu JS Kabylie CAF Champions League 2025/26. Waarabu wa Algeria walikuwa wanapewa nafasi kushinda hatua ya makundi, Uwanja wa Hocine Ait Ahmed na matokeo rasmi 0-0. Wakati Yanga SC ikipata pointi moja ugenini, Azam FC 0-1 Wydad Casablanca CAF Cofideration Cup. Matajiri wa Dar wamepoteza wakiwa nyumbani.

SOMA HII: Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions League/ Prince Dube afunga goli la ushindi New Amaan Complex

Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Bado hujashinda na SportPesa? Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

image

Yanga SC yaibana mbavu JS Kabylie CAF Champions League kimkakati

Yanga SC yaibana mbavu JS Kabylie CAF Champions League
Diarra kipa namba moja wa Yanga SC. Source: Yanga SC.

Licha ya kuwa ugenini, Yanga SC yaibana mbavu JS Kabylie CAF Champions League mbele ya mashabiki wao. Pedro Goncalves, Kocha Mkuu wa Yanga SC aliwaruhusu wapinzani kumiliki mpira.Waarabu wa Algelia waliliandama lango mithili ya nyuki waliambulia patubu.

JS Kabylie Yanga SC
63%Umiliki wa mpira37%
16Mashuti yaliyopigwa11
6Mashuti yaliyolenga lango3
7Kona0
0Kadi nyekundu0
3Kipa okoa hatari6
1Kadi ya njano2

SOMA HII: Yanga SC vs AS FAR 22/11/2025: Kazi imeanza, Wananchi watoa tamko zito

image

Kikosi cha JS Kabylie kilichoanza vs Yanga SC

Mlinda mlango
Hadid

Mabeki
Hamid
Madani
Belaid
F.Nechat

Viungo
Boudjemaa
Babar Sarr
Boudebouz

Washambuliaji
L.Akhrib
Mahious
Merghem

Kikosi cha Yanga SC kilichoanza dhidi ya JS Kabylie

Mlinda mlango

Diarra

Mabeki

Zimbwe Jr
Hamad Bacca
Dickson Job
Israel Mwenda

Viungo
Maxi Nzengeli
Duke Abuya
Pacome Zouzoua
Mudathir Yahya
Ecua

Mshambuliaji
Prince Dube

Matokeo na mechi ijayo

JS Kabylie 0-0 Yanga SC, Novemba 28,2025.

Yanga SC vs JS Kabylie, Februari 13,2026.

Msimamo wa kundi B CAF Champions League

jOB caf
Dickson Job beki wa Yanga SC vs JS Kabylie CAF Champions League. Source: Yanga SC.
TimuMechiPointiShindaSare
1. Al Ahly2411
2.Yanga SC2411
3. AS Far Rabat2101
4. JS Kabylie2001

SOMA HII: JS Kabylie vs Yanga SC CAF Champions League Novemba 28/ Lineups, H2H, livescore

image

Azam FC 0-1 Wydad Casablanca CAF Cofederation Cup

Azam FC Caf
Sadio Kanoute nyota wa Azam FC kwenye mchezo vs Wydad. Source: Azam FC.

Wawakilishi wa Tanzania kwenye CAF Cofideration Cup, Azam FC wamepoteza pointi sita. Kwenye mechi mbili walizoshuka uwanjani ugenini na nyumbani walipoteza. Mchezo wa Novemba 28,2025 ulikuwa ni wapili kwa Azam FC.

Florent Ibenge Kocha Mkuu wa Azam FC amesema kuwa wachezaji walijitoa kwa asilimia kubwa licha ya kukosa matokeo kwenye mchezo wao wa pili. Baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa New Amaan Complex ulisoma Azam FC 0-1 Wydad Casablanca ikiwa ni mchezo wa hatua ya makundi.

Bao la ushindi lilifungwa na Nordin Amrabat dakika ya 57 kipindi cha pili lilidumu mpaka mwisho wa mchezo ikiwa ni mechi ya pili Azam FC kupoteza baada ya kuanza ugenini kufungwa 2-0 dhidi ya AS Maniema.

Ibenge amesema wachezaji walifanya kazi kubwa ndani ya uwanja wanastahili pole licha ya kukwama kupata ushindi.

“Ninaweza kusema pole kwa wachezaji kwa kuwa walikuwa katika mchezo mzuri, walikimbia sana na mwisho tumekosa matokeo hivyo makosa tutafanyia kazi kwa mechi zijazo,”.

Msimamo wa kundi B Caf Confideration Cup 2025/26

TimuMechiPointiShindaSare
1. Wydad Casablanca2620
2. Maniema Union1310
3. Azam FC2000
4. Nairobi United1000

Ni timu mbili ambazo zitamaliza nafasi za juu zitasonga mbele hatua ya robo fainali. Ikitokea timu zikawa sawa katika pointi hapo mshindi atatazamwa kupitia h2h dhidi ya timu wanayolingana pointi. Tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa. Kwenye mchezo wa jana kiungo Aziz Ki mara baada ya mchezo kukamilika alipatwa na tatizo ma kuwahishwa hospitali kwa matibabu zaidi.

Hitimisho

Yanga SC yaibana mbavu JS Kabylie CAF Champions League 2025/26 ikiwa ugenini. Ni mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa katika hatua ya makundi. Matokeo hayo yanawafanya wanajangwani kuwa kwenye nafasi nzuri kutinga hatua ya makundi. Kutoka kundi B la CAF Champions League ni Al Ahly na Yanga SC zinapewa nafasi kupenya.


Share this: