Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions LeaguePrince Dubee
  • Prince Dube mshambuliaji wa Yanga SC amefunga goli la ushindi kwenye mchezo wa hatua ya makundi Uwanja wa New Amaan Complex.
  • Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions League Novemba 22,2025.
  • AS FAR Rabat ya Morocco rekodi imevunjwa ugenini kwa kupokea kichapo anga la kimataifa mchora ramani akiwa ni kiungo Mudathir Yahya.

Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions League matokeo rasmi ya mchezo wa kwanza hatua ya makundi. Wananchi wameanza kwa ushindi nyumbani mbele ya wenyeji wao waliokuwa katika mchezo wa kwanza kundi B. Prince Dube amevunja mwiko wa timu hiyo kutofungwa katika mechi 7 zilizopita za mashindano.

SOMA HII: Yanga SC vs AS FAR Rabat CAF Champions League ni leo Novemba 22 2025/ Matokeo, ratiba

Cheza sasa ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Bado hujashinda na SportPesa? Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

image

Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions League Zanzibar

Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions League
Prince Dube vs AS FAR Rabat. Source: Yanga SC.

Ubao wa Uwanja wa New Amaan Complex umesoma Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions League. Ukuta wa AS Far Rabat ulivunjwa kwa pasi ndefu ya kiungo Mudathir Yahya dakika ya 58. Prince Dube ambaye alikamilisha kazi kwa kufunga goli pekee la ushindi.

AS FAR Rabat kwenye mechi 7 za ushindani walikuwa hawajapoteza. Ushindi ilikuwa mechi 5 huku wakiambulia sare mbili. Huu unakuwa mchezo wa kwanza kuambulia kipigo wakiwa ugenini.

Kampeni za hatua ya robo fainali zimeanza kwa kasi huku Yanga SC kete ya kwanza wakikomba pointi tatu kundi B. Ushindi huo unawafanya wananchi kuongoza kundi kwa muda. AS Far  Rabat inashikilia mkia ikiwa haijakusanya pointi.

Mechi ya marudiano inatarajiwa kuchezwa Februari 6,2025. Katika mchezo ujao Yanga SC itakuwa ugenini. Pointi tatu zinatafutwa ili timu mbili zitinge hatua yar obo fainali.

SOMA HII: Yanga SC vs AS FAR 22/11/2025: Kazi imeanza, Wananchi watoa tamko zito

image

Goli la Prince Dube na maajabu yake

Prince Dube mfungaji wa goli la ushindi katika mchezo wa kwanza hatua ya makundi. Majabu ya Dube yamepatikana baada ya majaribio ya mara kwa mara kuzuiliwa na mlinda mlango wa AS FAR Rabat. Miongoni mwa jaribio ambalo alifanya Dube ilikuwa ni dakika ya 6.

Goli hilo alifunga kipindi cha pili akitumia pasi ya Mudathir Yahya. Nyota mwingine aliyefanya jaribio kali ilikuwa ni Maxi Nzengeli dakika ya 30. Uimara wa kipa wa AS FAR Rabat uliweka lango salama dakika 45 za kipindi cha mwanzo.

Msimamo upo namna hii

pACOME VS as
Pacome kiungo wa Yanga SC vs AS FAR Rabat. Source: Yanga SC.

1. Yanga SC pointi 3 mechi 1
2. JS Kabylie pointi 0 mechi 0
3. Al Ahly pointi 0 mechi 0
4. AS FAR Rabat pointi 0 mechi 1

Kikosi cha Yanga SC kilichoanza dhidi ya AS FAR Rabat

Zimbwe Zenji
Zimbwe Jr beki wa Yanga SC alianza kikosi cha kwanza dhidi ya AS FAR Rabat. Source: Yanga SC.

Djigui Diarra

Israel Mwenda

Zimbwe Jr

Dickson Job

Ibrahim Bacca

Duke Abuya

Maxi Nzengeli

Mudathir Yahya

Prince Dube

Pacome Zozoua

Celectin Ecua

Wachezaji wa akiba

Aboutwalib Mshery, Bakari Nondo, Boka, Balla Conte, Sheikhan Khamis, Lassine Kouma, Doumbia Mo, Edmund John, Boyel.

Kikosi cha AS Far Rabat kilichoanza dhidi ya Yanga SC

Tagnaouti

Bach

Abdelhamid

Louadni

Carneiro

Derrag

Hrimat

Hammoudan

Slim

Slim

Ait Ouarkhane

Al Fahli

Wachezaji wa akiba

El Khayati, Mendy, Bouriga, Khabba, Habessi, El Bouchoali, Ech Chemmakh, Ait Khassou, Hadraf.

image

Hitimisho

Yanga SC 1-0 AS FAR Rabat CAF Champions League imeonesha ukubwa wa timu za ukanda wa Afrika Mashariki. Nyota wa mchezo Prince Dube amepeleka kilio kwa AS Far Rabat. Mudathir alishindwa kujizuia alishangilia kwa nguvu baada ya goli hilo kufungwa.

Share this: