- Nchini Morocco Historia inaendelea kuandikwa kupitia atika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025).
- Mashindano hayo kwa sasa yameingia hatua ya mtoano, ambapo timu mbalimbali zinapambana kusaka tiketi ya hatua ya mtoano.
- Kwa mara ya kwanza timu ya Taifa ya Tanzania nayo imekata tiketi ya kufuzu hatua hiyo kwa nafasi ya ‘best looser’
- Taifa Stars itavaana na Morocco katika mchezo wa Morocco vs Tanzania unaotarajiwa kupigwa siku ya Jumapili.
Historia inaendelea kuandikwa nchini Morocco katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025). Mashindano hayo kwa sasa yameingia hatua ya mtoano ambapo timu mbalimbali zinapambana kusaka tiketi ya mashindano hayo. Katika hali ya upekee matokeo ya sare ya Tanzania 1-1 Tunisia, yanaifanya Tanzania kwa mara ya kwanza kuandika rekodi ya kufuzu hatua ya 16 bora. Tanzania inaungana na timu nyingine 3 kuunda timu 4 ambazo zimefuzu kama ‘best looser’. Makala hii inaangazia timu ambazo zimefuzu hatua ya 16 bora.
SOMA HII PIA: AFCON 2025: Hizi hapa nchi 5 zilizotolewa mapema
Je, hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.
AFCON 2025 timu hizi zimefuzu moja kwa moja
Mpaka sasa baadhi ya timu zimefanikiwa kufuzu moja kwa moja kwa kumaliza kwenye nafasi za juu, (Nafasi ya 1 na ya 2), kwenye makundi yao.
Misri

Mali

Afrika Kusini

Morocco

Nigeria

Tunisia

Timu ambazo zimefuzu kama ‘Best Looser’
Tanzania ndiyo timu pekee ambayo imethibitisha kufuzu kwa mfumo wa best looser, zipo timu nyingine 3 ambazo zitafuzu kama best looser lakini inasubiriwa mechi zao za mwisho kuamua nani anafuzu moja kwa moja, na nani anafuzu kama best looser. Timu hizi tatu zitatoka katika kundi D, E na F.
SOMA HII ZAIDI: AFCON 2025 matokeo na ratiba hii hapa/ Msimamo, live scores
Timu zinazosubiri mechi za mwisho ni

Group D: Senegal, DR Congo, Benin
Group E: Algeria, Burkina Faso, Sudan
Group F: Cameroon, Ivory Coast, Mozambique
SOMA HII PIA: Afcon 2025: Hawa hapa wachezaji 10 wanaolipwa pesa nyingi
Taifa Stars kuwavaa Morocco 16 bora mechi Morocco vs Tanzania

Kwa kufanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora, Timu ya Taifa ya Tanzania inatarajiwa kuvaana na Morocco katika hatua hiyo. Mchezo huo unatarajiwa kupigwa jijini Rabat kwenye Uwanja wa Prince Moulay Abdellah. Hii inatarajiwa kuwa Jumapili ya Januari 4, mwaka 2026.

