Yanga SC vs AS FARYanga SC vs AS FAR
  • Hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika itaanza punde tu, baada ya kukamilika kwa ratiba ya mechi za kimataifa.
  • Yanga SC vs AS FAR CAF mchezo utakaopigwa Novemba 22, 2025 umeanza kuwa gumzo.
  • Hii ni kutokana na ubora na utajiri mkubwa, wa historia kwa timu hizi katika mashindano ya kimataifa.

Hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika inatarajia kuanza punde tu, baada ya kukamilika kwa ratiba ya mechi za kimataifa. Yanga SC vs AS FAR CAF mchezo ambao utapigwa siku ya tarehe 22 Novemba 2025, umeanza kuwa gumzo. Hii ni kutokana na ubora na utajiri mkubwa, wa historia kwa timu hizi katika mashindano ya kimataifa. Uongozi wa kikosi cha Yanga SC chini ya kocha mkuu mpya, Pedro Goncalves umejichimbia kuwaandalia waarabu dozi.

SOMA HII PIA: Makundi Klabu Bingwa Afrika CAF 2025/26 haya hapa | Simba SC na Yanga SC zapewa waarabu

Cheza sasa ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Je, bado hujashinda na SportPesa? Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

image

Yanga wamepangwa dhidi ya timu gani makundi

Makundi Klabu Bingwa Afrika CAF
Droo-ya-Makundi-Klabu-Bingwa-Afrika

Katika droo ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika 2025/26, ambayo yalipangwa nchini Afrika Kusini Novemba 3, mwaka huu. Yanga SC wamefanikiwa kupangwa kwenye Kundi B pamoja na timu za Al Ahly ya Misri, AS FAR ya Morocco na JS Kabylie ya Algeria. Makundi mengine ni kama ifuatavyo:

Kundi A

RS Berkane kutoka Morocco

Pyramids FC kutoka Misri

Rivers United kutoka Nigeria

Power Dynamos kutoka Zambia

Kundi C

Mamelodi Sundowns kutoka Afrika Kusini

Al Hilal kutoka Sudan

MC Alger kutoka Algeria

St Eloi Lupopo ya Congo

Kundi D

ES Tunis ya Tunisia

Simba SC kutoka Tanzania

Petro Luanda ya Angola

Stade Malien ya Mali

SOMA HII ZAIDI: Tanzania NBC Premier League table & standings 2025-26 season

Hatua ya makundi itaanza kutimua vumbi lini?

Kundi la Yanga SC
Kundi la Yanga SC

Hatua ya makundi ya CAF Champions League yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 21,2025, kwa michezo yam kondo wa kwanza. Hatua hii itaendelea mpaka kila timu itakapomaliza mechi zake 6, yaani 3 za ugenini na 3 za nyumbani. Kutoka kwenye kila kundi zinatafutwa timu mbili, ambazo zitasonga hatua ya robo fainali.

Safari ya Yanga SC mpaka kufika hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika?

Yanga SC --- Silver Strikers CAF Champions League Oktoba --
Yanga SC vs Silver Strikers CAF Champions League Oktoba

Yanga SC kutoka Tanzania ilianzia katika hatua ya awali. Katika hatua hiyo walicheza mechi nne, mbili ugenini na mbili ikiwa nyumbani. Hatua ya kwanza ilianza dhidi ya Wiliette SC kutoka nchini Angola na kufanikiwa kupata ushindi wa jumla wa magoli 5-0.

Hatua ya pili ya awali Yanga SC iliyokuwa inanolewa na kocha Romain Folz ilivaana na Silver Striker ya Malawi. Ugenini ilipoteza kwa kufungwa goli 1-0, katika mchezo ulioondoka na kibarua cha Folz. Kwenye mchezo wa marudiano uliopigwa Uwanja wa Mkapa, Yanga SC ilifanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-0 na ikasonga mbele kutinga hatua ya makundi.

SOMA HII PIA: Ratiba ya Yanga SC 2025/26 NBC Premier League, CAF Champions League/ Live scores

Yanga SC kuisaka Robo Fainali Zanzibar

Uongozi wa Yanga SC kupitia kwa Ofisa Habari wake, Ali Kamwe umeutangazia Umma wa soka na mashabiki wake kuwa mechi zao zote tatu za kimataifa hatua ya makundi zitapigwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Huu ndio unatarajia kuwa uwanja wao wa nyumbani. Yanga SC vs AS FAR ndiyo karata ya kwanza kwa Yanga Novemba 22, mwaka huu.

Ratiba kamili ya Yanga SC hatua ya makundi CAF Champions League

Yanga SC vs AS FAR inatarajiwa kuchezwa Novemba 22, 2025

JS Kabylie vs Yanga SC inatarajiwa kuchezwa Novemba 28, 2025

Al Ahly vs Yanga SC inatarajiwa kuchezwa Januari 23, 2026

Yanga SC vs Al Ahly inatarajiwa kuchezwa Januari 30, 2026.

AS FAR vs Yanga SC inatarajiwa kuchezwa 6, Februari 2026.

Yanga SC vs JS Kabylie inatarajiwa kuchezwa Februari 13,2026.

Yanga SC vs AS FAR, Kocha Pedro awaandalia Waarabu dozi

Yanga SC vs AS FAR CAF
Kocha Pedro

Kwa kutambua uzito wa timu ambazo wanatarajia kuvaana nazo na mchezo dhidi ya AS FAR, kocha mkuu wa Yanga, Pedro ameendelea kuwapa mazoezi mazito mastaa wake waliosalia kambini. Katika ripoti mbalimbali ambazo zimetolewa na uongozi wa timu hiyo,zinaonyesha mazoezi makali yakiendelea Uwanja wa KMC, Dar es Salaam.

Hitimisho

Kuelekea mchezo wa Yanga SC vs AS FAR CAF, Licha ya ubora wa AS FAR ambao wanauonyesha katika ligi ya Morocco wakishika nafasi ya pili. Bado umadhubuti wa Yanga SC kwenye mashindano ya kimataifa umezidi kuimarika. Misimu miwili iliyopita walicheza fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika. Mashabiki wao wanatamani kuona timu inaandika rekodi nyingine kubwa zaidi msimu huu, hasa baada ya kuishia makundi msimu uliopita.

Share this:

By Joel Thomas

Joel Thomas is a Tanzanian sports writer with a BSc (Education) from Mwenge Catholic University. He spent 4 years at Global Publishers and is in his second year with SportPesa, covering football and betting education for local fans. Anapenda soka na anaandika kwa uwajibikaji.